user_mobilelogo

Party Emblem

Party Flag

 

Youth League

Contact us


Communist Party Marxist - Kenya (CPM-K)
This email address is being protected from spambots. You need JavaScript enabled to view it.
P.O Box 101011-00101 Nairobi, Kenya.
 

Let's Get Social

          

 

Related Social Links

 Revolutionary Youth League (RYL)
   
 Revolutionary Student Commission
    
 Revolutionary Women League
 Pio Gama Pinto Institute 

Support CPM-K 

membership

Publications

 

 

 

 Grab a Copy

 

CPM-K Memberships

 

 

 

 

 

 

 

 

 

Mau Mau

Mau Mau, jeshi la Uhuru na Mashamba

Kilele cha mapambano dhidi ya ukoloni-mkongwe

Jazanda ya wazalendo na uzalendo

Mau Mau, mashujaa halisi wa nchi yetu

Wakakataa kutembea katika njia ya kina Jomo Kenyatta

Njia ya wasabili ya kuomba uhuru wa kuomba

Njia ya kutegemea adili ya wagandamizaji

Njia ya kuongozwa na masilahi ya ulafi na uroho

Njia ya kukana mapambano ya silaha katika hali ya ufashisti

Mau Mau wakulima na wafanyikazi wa Kenya

Wanaume kwa wanawake wazee kwa vijana

Walichagua barabara ya kimapinduzi ya uhuru

Mau Mau waliokula kiapo cha ukombozi

Kiapo cha kuwaunganisha na kuwashikanisha kwa mapambano

Mapambano ya kupigania mashamba na uhuru wetu

Mapambano ya kupigania heshima na utu wa mtu mweusi

Mapambano ya demokrasi na haki za binadamu

Mapambano ya kuung'oa ukoloni nchini kwetu

Maelfu kwa maelfu ya wazalendo wa Kenya

Waliowacha kila kitu na kuitikia mwito

Mwito wa kujitoma milima Kenya na Nyandarua

Mwito wa kusambaa katika miji na vijiji vya nchi yetu

Kuendeleza vita vya kigorila dhidi ya wakoloni na vibaraka vyao

Waliovumilia njaa na kiu na baridi na upweke na dhiki tilatila

Wakajasiri kuwindwa na kukamatwa na kuhamishwa

Waliokuwa tayari kuvumilia kukamatwa na kufungwa

Mau Mau, maelfu kwa maelfu waliwawa na wakoloni

Mau Mau, ni wangapi mashujaa wetu waliyonyongwa!

Mau Mau, kiboko cha makaburu na mahomugadi

Mau Mau, kwa damu yenu, kwa kujitolea mhanga kwenu

Enyi wananchi wakereketwa wa taifa letu

Kwa msimamo wenu

Kwa mwelekeo wenu

Kwa harakati zenu

Kwa vita sahihi mlivyopigana

Tuko pahali tulipo sasa, hatua kubwa mbele

Ukoloni-mkongwe haupo tena nasi, mliukwamua Mau Mau

Kwenu Afrika ikapata mfano mzuri wa kuiga

Mfano wa kupigania ukombozi kwa kutumia silaha

Mau Mau, Jeshi la uhuru na Mashamba

Na sisi leo

Lazima tupambane kwa vyovyote vile

Tujikaze kisabuni

Mateso na majaribu ya kila aina

Tunayaona

Na tutaendelea kuyaona

 

Mau Mau

Vilikuwa vita vya kupigania uhuru wa kitaifa

Vita vya wananchi na wananchi kwa ajili ya wananchi

Navyo vita vya wananchi vilizaa mashujaa wengi, wengi sana

Mashujaa waliochipuka katika msitari wa mbele

Mashujaa walioteuliwa na ari na shauku ya kujitolea mhanga

Kujitolea mhanga kutumikia vita vya ukombozi

Mashujaa waliodhihirisha ujemedari na uhodari

Wa kuongoza jeshi lililokuwa la wananchi wa Kenya

Mashujaa waliokuwa mashuhuri katika uwanja wa vita

Kwa usanii wa kuzalisha hila na mbinu za kuwachapa maadui

Mashujaa wa siasa na itikadi ya wanaonyanyaswa

Waliohamasisha umma kwa maneneo na vitendo vyao

Mashujaa wa kutetea haki na ukweli na maslahi ya wengi

Waliochagua kuishi maisha ya utu ya kupinga dhuluma

Mashujaa kwa mapenzi ya nchi yetu na ukombozi wake

Kwa maendeleo ya Kenya na furaha  ya kila raia

Kwa imani na amani ya wanaonyonywa na kunyanyaswa

Mashujaa waliokuwa wakipiga konde nyoyo kila wakati

Waliopambana dhidi ya kulegalega na kukata tamaa

Mashujaa ambao baada ya kukamatwa na wakoloni

Wakiwa mikononi mwa makaburu na mahomugadi

Wakiteswa katika magereza ya wadhalimu wa nchi yetu

Katikati ya ufashisti wa dola la Waingereza

Walivumilia yote kwa ujasiri usiyo na kifani

Walikataa kusaliti kiapo cha kupigania uhuru

Wakadinda kukana vita vya haki vya ukombozi wa Kenya

Wasikubali kutoboa siri wala kusaliti makomredi wao

Na hata waliponyongwa na kuuawa kinyama kabisa

Mashujaa wetu walikufa kwa fahari

Wakawawachia wakoloni na vibaraka wao aibu ya milele

Ni wengi mashujaa wa Mau Mau, wengi sana

Kwani Mau Mau ni wanati, wananchi wazalendo wakereketwa

Mau Mau, ushujaa wa mamilioni

Ya wakulima na wafanyikazi

Wanaume kwa wanawake wazee kwa vijana

Ambao kwa moyo wa harambee uzalendo na kujitegemea

Walifunga sura  ya ukoloni-mkongwe katika nchi yetu

Na sisi leo

Lazima tupambane kwa vyovyote vile

Tujikaze kisabuni

Mateso na majaribu ya kila aina

Tunayaona

Na tutaendelea kuyaona

 

Kimaathi

Dedan Kimaathi

Dedan Kimaathi wa Waciuri

Mkuu wa jeshi la Uhuru na Mashamba

Kati ya majemedari wa Mau Mau Kimaathi ali ni gogo

Baina ya mashujaa wa uhuru hakika Dedan Kimaathi ni nyota

Nyota iliyoonekana na inayoonekana katika kila pembe ya Kenya

Nyota inayong'aang'aa Afrika kuonyesha barabara sahihi

Barabara ya kimapinduzi ya kuelekea kwa uhuru

Nyota mashuhuri Afrika na hata duniani kote

Kwa wanaonyonywa na kugandamizwa

Oh pande la mwana wa Kenya, ndugu yetu mpendwa Kimaathi

Ni maneno gani tutayatumia  ewe mwana wa Waciuri

Hata tukaeleza  sifa zako tilatila kwa kikamilifu?

Ninashindwa hata kupata nahau bora

Za kuandika kuhusu Mkuu wa Jeshi la Uhuru na Mashamba

Pengine niseme tu kuwa Kimaathi alikuwa mtu

Alikuwa mtu Kimaathi, mtu kama sisi

Alikuwa na mamaye na babaye na bibiye na babuye

Alikuwa na jamaaze, damuye, kama sisi

Alikuwa na mke, mke aliempenda sana, tena sana

Kimaathi alikuwa kijana, kijana  kama sisi

Kijana alietambua jukumu lake kama mwananchi mzalendo

Mtu ambae alifahamu yu mtu kwa maneno na matendo

Kimaathi, maana ya mapenzi kwa nchi yako na watu wake

Kimaathi, mfano halisi wa ushujaa wa kimapinduzi

Ushujaa wa umma uhodari wa maslahi ya wanaogandamizwa

Kimaathi, twasira na jazanda ya kujitolea mhanga

Kwa uhuru na ukombozi wa kitaifa

Kati ya wasanii wa hila na mbinu ya vita vya kigorila

Kimaathi wa Waciuri anatajika kama msanii mkubwa

Kati ya majina yaliyokuwa yakiogopewa na wakoloni

Jina la Dedan Kimaathi lilikuwa namba wani

Kimaathi aliwafanya makaburu kujikojolea na kujiharia

Wanyonyaji wakashindwa kula manyonyaji yao kwa amani

Wangapi walowezi walifungasha na kuondoka

Kwa kuogopa Kimaathi, asakari hodari wa Mau Mau!

.....ahhhh! lakini nani asiemfahamu Kimaathi nchini!

Ni mwananchi gani mzalendo ambae hajui Mau Mau!

Ni historia gani ya Kenya hiyo ambayo haitaji Mau Mau!

Ni mashujaa gani wa Kenya unawajua kama humjui Kimaathi!

Hakika katika kuandika historia sahihi ya taifa letu

Hatutawasamehe kina Ndirangu Mau milele

Kina Ndirangu Mau- mahomugadi waliyomsaliti shujaa wetu

Kina Ndirangu Mau- kina Kenyatta na Moi wenye dola la kisaliti

Kina Ndirangu Mau- wanyonyaji wa wakulima na wafanyikazi

Kina Ndirangu Mau- vibaraka wa mabeberu

Kina Ndirangu Mau- wanaopinga ukombozi wa taifa letu

Tutawasemehe vipi kwa kuendelea kukataa kumzika Kimaathi!?

Mnamo tarehe 18  Februari, 1957

Katika Jela ya Nairobi

Dedan Kimathi wa Waciuri, shujaa mkuu wa Kenya

Alinyongwa na wakoloni wa Waingereza

Alinyongwa baada ya mateso ya kifashisti ya kina Ian Henderson

Alinyongwa huku akipambana akiwa na pingu mikononi

Shujaa wa nchi yetu alikufa akipigana

Mwili wa Kimaathi ulitupwa na wakoloni

Katika Jela ya Kamiti

Na hadi wa leo

Mazishi ya Mzalendo Kimathi

Yanangojea kufanywa, tukumbuke

Na sisi leo

Lazima tupambane kwa vyovyote vile

Tujikaze kisabuni

Mateso na majaribu ya kila aina

Tunayaona

Na tutaendelea kuyaona

Mwamdawiro Mghanga, Mwenyekiti wa CPK

                                                            Jela Kuu ya Kibos    04-06-198

 

STATEMENT OF THE CENTRAL ORGANISING COMMITTEE OF THE COMMUNIST PARTY MARXIST KEN...
30 Jun 2026 10:27

  WHO MURDERED COMRADE PETER MASINDE?   29 June 2026   The Central Organising Committee of the Communist Party Marxist Kenya extends its deepest condolences and revolutionary solidarity to the family, friends, and fellow workers of Comrade Peter Masinde, a militant warehouse worker whose life was cut short under conditions that expose the brutality of exploitation in Kenya’s neocolonial economy.   Today, the Communist Party Marxist Kenya joined the Warehouse Workers Committee and hundreds of workers outside the gates of the National Cereals and Produce Board warehouses in Shimanzi [ ... ]

Read more
STATE TERROR HAS NAMES. SO DO ITS VICTIMS.
30 Jun 2026 10:26

  A TRIBUTE OF THE COMMUNIST PARTY MARXIST KENYA TO THOSE KILLED, DISAPPEARED, ABDUCTED, TORTURED AND IMPRISONED DURING THE RUTO REGIME   SAY THEIR NAMES     The Kenyan flag stands as a symbol of defiance against comprador rule.   Our martyrs never die.   Wrapped in the patriotic Kenyan flag, they live on in the struggle and in the memory of the people.   The blood of our martyrs shall forever bear witness to the sacrifices made in the fight for justice and liberation.   #JusticeForOurMashujaas   History is not written only by those who occupy the highest offices of th [ ... ]

Read more
ON THE DEGENERATIVE ROLE OF NGO ACTIVISM, OPPORTUNISM, AND POLITICAL SABOTAGE WI...
11 Jun 2026 09:26

  Mathare Social Justice Centre, Gacheke Gachihi, Waringa Wahome and the Politics of Celebrity Activism The Central Organising Committee of the Communist Party Marxist Kenya considers it necessary to openly address the increasingly negative role played by sections of the so called social justice movement, particularly individuals associated with Mathare Social Justice Centre, whose conduct has come to embody the politics of celebrity activism, NGO dependency, opportunism, and hostility towards revolutionary organisation. This statement is not about personalities. It is about politics. It i [ ... ]

Read more
THE ESCALATING CRISIS OF FEMICIDE IN KENYA
02 Jun 2026 08:50

  STATEMENT BY THE STEERING COMMITTEE OF THE REVOLUTIONARY WOMEN’S LEAGUE   June 1, 2026    The Revolutionary Women’s League extends its deepest condolences to the families, friends and communities of all women whose lives have been stolen through femicide. We mourn every daughter, every mother, every sister, every wife, every domestic worker, every student, every worker, every queer woman and every woman whose life has been violently cut short.   We stand in solidarity with all those who continue to carry the pain of these losses. We do so not only as women, but as members of  [ ... ]

Read more