user_mobilelogo

Party Emblem

Party Flag

 

Youth League

Contact us


Communist Party Marxist - Kenya (CPM-K)
This email address is being protected from spambots. You need JavaScript enabled to view it.
P.O Box 101011-00101 Nairobi, Kenya.
 

Let's Get Social

          

 

Related Social Links

 Revolutionary Youth League (RYL)
   
 Revolutionary Student Commission
    
 Revolutionary Women League
 Pio Gama Pinto Institute 

Support CPM-K 

membership

Publications

 

 

 

 Grab a Copy

 

CPM-K Memberships

 

 

 

 

 

 

 

 

 

Nawasalimu Makada wote wa Chama Cha Kimonunisti Kenya na Wageni wote waalikwa. Siku ya leo ambayo ni siku muhimu sana yakuadhimisha na kuwasherehekea wafanyikazi wote duniani. 

Leo tunajumuika hapa Kisumu lakini sisi ni baadhi tu ya wavujajasho wengi waliojumuika katika kila Pembe ya dunia kusherehekea nguvu Kazi ya wavujajasho duniani.

Lakini, Kuna nini  chakusheherekea kwa  wafanyikazi ? Wakati mabilioni ya wafanyikazi wanaendelea kukandamizwa na mfumo wa kiimla wa ubepari. Mfanyikazi hana chochote chakusheherekea katika jamii yenye inaongozwa na  uimla wa mtaji wakibinafsi dhidhi ya maslahi ya wanaotengeneza mtaji huo.

Jamii yetu imegawanyika baina ya wavunajasho wachache wanao miliki nyenzo za uzalishaji na wanaozitumia kunyonya nguvukazi ya wavujajasho wengi ambao wanaendelea kuishi maisha ya kichochole.

Wafanyikazi wa Kenya kama wafanyikazi wengine wameenedelea kukandamizwa kwa kulipwa Mishahara duni na isiyoweza kukimu mahitaji yao, wafanyikazi wameendelea kufanya kazi masaa zaidi ya yale yanayotakikana na sheria za kufanya kazi duniani. Mazingira yakufanya Kazi yamezorota na wafanyikazi wengi wanapata ajali na hata magonjwa kutokana na Mazingira duni yakufanya kazi. 

Serikali ya Kenya haijaweka mikakati yoyote yakulinda maslahi ya wafanyikazi na hata kuongeza nguvukazi ya taifa lenye lina watu waliohitimu katika tajriba tofauti na ambao bado hawajapata kazi kwa sababu yakutoendeleza viwanda na kilimo ambayo ndiyo nguzo msingi ya nchi yeyote inayotaka kujiendeleza.

Mashirika yakimataifa kama Benki ya Dunia na IMF( International Monetary Fund) yameendelea kushinikiza matakwa ya ulibarali mamboleo ambayo yamekua na madhara makubwa kwa wafanyikazi na maisha ya mvujajasho wa Kenya.

Serikali hii ya kiimla pia imeendelea kusimamisha na kupinga juhudi zozote za wafanyikazi kuungana na kujitetea. Polisi wametumika kuwapiga wafanyikazi wakati wanapo fanya migomo na serikali imekataa kufuata mikataba ya makubaliano na wafanyikazi wa umma.

Vyama vya wafanyakazi na viongozi wa vyama hivi pia wamenunuliwa ili kulegeza kamba katika mapambano ya wafanyikazi. Sisi wakomunisti tukona na jukumu lakuenda miongoni  mwa wafanyikazi hawa na kuwapa mwamko Mpya wa kimawazo ili wabadilishe mambo yalivyo.

Sisi wakomunisti tunafaa kuendelea na kazi yakujenga vyama hivi vya wafanyikazi na kuleta mawazo ya kimapinduzi kwa wafanyikazi ili waelewe   uwezo walio nao. 

 Ingawaje,  vyama hivi vingine vimeshikiliwa na mabepari mchwara wanaotumia uongozi wao ili kuendelea kujinufaisha kibinafsi kama katibu mkuu wa COTU(Confederation of Trade Union) Bwana Francis Atwoli. Viongozi hawa ni kupe wanaonyonya jasho la wafanyikazi wakenya na lazima tuwapinge ki itikadi na tuwang'oe ili turejeshe hadhi ya vyama vya wafanyikazi wakati wa wazalendo kama Makhan Singh, Fred Kubai, Bildad Kaggia na Chege Kibacia.

Wakomunisti pia tunajukumu la kujenga Chama cha Kisiasa cha wafanyikazi CPM-K kwani tunapigana kuchukua uongozi na kujenga uimla wa wafanyikazi dhidhi ya wanaomilki mtaji, hii ndio njia yakujenga mfumo wa usoshialisti ili kuelekea katika mfumo wa kikomunisti ambapo hakuna ukandamizaji baina ya binadamu na binadamu mwingine.

Chama Chetu CPM-K ndicho kitapeleka harakati na gurudumu la wafanyikazi mbele ya mambo mengine ambayo vyama vingine vya wafanyikazi haviwezi kutekeleza. 

Makada wote wa Chama wanajukumu la kihistoria na la kijamii kujenga Chama mahali wanapofanyia kazi ili kuleta mawazo yakimapinduzi kwa wafanyikazi wengine, Chama chetu nicha wafanyikazi na lazima tukijenge miongoni mwa wafanyikazi wenyewe.

Chama chetu kitajaribu kuleta pia Wakulima na wavujajasho wengine katika jamii ili kuikomboa Kenya na dunia kutokana na maovu ya ubepari na ubeberu. Mapigano ya kwanza yakatukua dhidhi ya mabepari wa nyumbani wanaoendeleza maslahi ya mabeberu na mabepari wa nje kwa kufanya kazi ya kibaraka na kutumia vyombo vya dola venye vinamilikiwa na mabepari wa nje ili kukandamiza jamii.

Nawatakia mazungumzo yenye fanaka katika mkutano wa leo wakuadhimisha siku hii na tuendele kujenga Chama cha wafanyikazi.

 

Yadumu Mapambano ya wafanyikazi !!!

Idumu harakati za kujenga Usoshalisti!!!

Kidumu Chama Cha Wafanyikazi CPM-K !!!

Mwaivu Kaluka.

Mwenyekiti Wa Chama Cha Kikomunisti Umaksi - Kenya.

STATEMENT OF THE CENTRAL ORGANISING COMMITTEE OF THE COMMUNIST PARTY MARXIST KEN...
30 Jun 2026 10:27

  WHO MURDERED COMRADE PETER MASINDE?   29 June 2026   The Central Organising Committee of the Communist Party Marxist Kenya extends its deepest condolences and revolutionary solidarity to the family, friends, and fellow workers of Comrade Peter Masinde, a militant warehouse worker whose life was cut short under conditions that expose the brutality of exploitation in Kenya’s neocolonial economy.   Today, the Communist Party Marxist Kenya joined the Warehouse Workers Committee and hundreds of workers outside the gates of the National Cereals and Produce Board warehouses in Shimanzi [ ... ]

Read more
STATE TERROR HAS NAMES. SO DO ITS VICTIMS.
30 Jun 2026 10:26

  A TRIBUTE OF THE COMMUNIST PARTY MARXIST KENYA TO THOSE KILLED, DISAPPEARED, ABDUCTED, TORTURED AND IMPRISONED DURING THE RUTO REGIME   SAY THEIR NAMES     The Kenyan flag stands as a symbol of defiance against comprador rule.   Our martyrs never die.   Wrapped in the patriotic Kenyan flag, they live on in the struggle and in the memory of the people.   The blood of our martyrs shall forever bear witness to the sacrifices made in the fight for justice and liberation.   #JusticeForOurMashujaas   History is not written only by those who occupy the highest offices of th [ ... ]

Read more
ON THE DEGENERATIVE ROLE OF NGO ACTIVISM, OPPORTUNISM, AND POLITICAL SABOTAGE WI...
11 Jun 2026 09:26

  Mathare Social Justice Centre, Gacheke Gachihi, Waringa Wahome and the Politics of Celebrity Activism The Central Organising Committee of the Communist Party Marxist Kenya considers it necessary to openly address the increasingly negative role played by sections of the so called social justice movement, particularly individuals associated with Mathare Social Justice Centre, whose conduct has come to embody the politics of celebrity activism, NGO dependency, opportunism, and hostility towards revolutionary organisation. This statement is not about personalities. It is about politics. It i [ ... ]

Read more
THE ESCALATING CRISIS OF FEMICIDE IN KENYA
02 Jun 2026 08:50

  STATEMENT BY THE STEERING COMMITTEE OF THE REVOLUTIONARY WOMEN’S LEAGUE   June 1, 2026    The Revolutionary Women’s League extends its deepest condolences to the families, friends and communities of all women whose lives have been stolen through femicide. We mourn every daughter, every mother, every sister, every wife, every domestic worker, every student, every worker, every queer woman and every woman whose life has been violently cut short.   We stand in solidarity with all those who continue to carry the pain of these losses. We do so not only as women, but as members of  [ ... ]

Read more